Robo Mwezi

Tekst
Loe katkendit
Märgi loetuks
Kuidas lugeda raamatut pärast ostmist
Šrift:Väiksem АаSuurem Aa

Table of Contents







Cover







Title







Copyright







Indice







Prologo







Sura ya kwanza







Sura ya pili







Sura ya tatu







Sura ya nne







Sura ya tano







Sura ya Sita







Sura ya Saba







Sura ya nane







Sura ya Tisa







Sura ya Kumi







Sura ya kumi na moja







Sura ya kumi na mbili







Sura ya kumi na tatu







Sura ya kumi na nne







Sura ya kumi na tano







Sura ya kumi na sita







Sura ya kumi na saba







Sura ya kumi na nane







Sura ya kumi na tisa







Sura ya ishirini










Robo Mwezi







Watumishi wa Campoverde









Imetafsiriwa na Kennedy Langat









Hakimiliki © 2019 M.G. Gullo – M. Longo







Picha ya jalada na michoro iliundwa na kuahiririwa na Massimo Longo







Haki zote zimehifadhiwa







ISBN







ISBN-13:











JEDWALI YA YALIYOMO













Sura ya Kwanza


Anaepuka nikijaribu kumkumbatia...

Sura ya Kwanza


Anaepuka nikijaribu kumkumbatia...



















Sura ya Pili


Mnong'ono wa baridi ulikuwa ukimsumbua

Sura ya Pili


Mnong'ono wa baridi ulikuwa ukimsumbua



















Sura ya Tatu


Aligundua kuwa mvulana huyo alikuwa ametishika, na akaangua kicheko


Sura ya Tatu


Aligundua kuwa mvulana huyo alikuwa ametishika, na akaangua kicheko


Sura ya Tatu


Aligundua kuwa mvulana huyo alikuwa ametishika, na akaangua kicheko




















Sura ya nne


Sauti ilikuwa ikinong'oneza masikioni mwake maneno kwa lugha isiyojulikana

Sura ya nne


Sauti ilikuwa ikinong'oneza masikioni mwake maneno kwa lugha isiyojulikana



















Sura ya Tano


Anakabiliwa na kitu cha kuogofya

Sura ya Tano


Anakabiliwa na kitu cha kuogofya



















Sura ya Sita


Hakuweza kutoa matamshi hayo kutoka kwa kichwa chake

Sura ya Sita


Hakuweza kutoa matamshi hayo kutoka kwa kichwa chake



















Sura ya Saba


Wahusika wasioeleweka waliwashwa na sauti ya kutuliza


Sura ya Saba


Wahusika wasioeleweka waliwashwa na sauti ya kutuliza


Sura ya Saba


Wahusika wasioeleweka waliwashwa na sauti ya kutuliza




















Sura ya Nane


Tafakari ya picha hiyo mbaya

Sura ya Nane


Tafakari ya picha hiyo mbaya



















Sura ya Tisa


Ngazi isiyo na mwisho

Sura ya Tisa


Ngazi isiyo na mwisho



















Sura ya Kumi


Alihisi kama angeweza kutoboa mbingu kwa mikono yake wazi

Sura ya Kumi


Alihisi kama angeweza kutoboa mbingu kwa mikono yake wazi



















Sura ya Kumi na Moja


Wazo hili liliendelea kuitesa royo yake

Sura ya Kumi na Moja


Wazo hili liliendelea kuitesa royo yake



















Sura ya Kumi na Mbili


Ilimkumbusha kinywaji cha vitunguu vya kiberiti

Sura ya Kumi na Mbili


Ilimkumbusha kinywaji cha vitunguu vya kiberiti



















Sura ya Kumi na Tatu


Alishuka kutoka angani akikokota mawingu yake meusi

Sura ya Kumi na Tatu


Alishuka kutoka angani akikokota mawingu yake meusi



















Sura ya Kumi na Nne

 Alishuka chini ya wingu

Sura ya Kumi na Nne

 Alishuka chini ya wingu


















Sura ya Kumi na Tano


Kama kwamba alimezwa na Dunia

Sura ya Kumi na Tano


Kama kwamba alimezwa na Dunia



















Sura ya Kumi na Sita


Ghafula kelele za ajabu zilisikika kama za kigugumizi cha kina

Sura ya Kumi na Sita


Ghafula kelele za ajabu zilisikika kama za kigugumizi cha kina



















Sura ya Kumi na Saba


Alikuwa akitembea vizuri wakati alipovuka kizingiti

Sura ya Kumi na Saba


Alikuwa akitembea vizuri wakati alipovuka kizingiti



















Sura ya Kumi na Nane


Makucha yaliingia ndani ya ngozi yake

Sura ya Kumi na Nane


Makucha yaliingia ndani ya ngozi yake



















Sura ya Kumi na Tisa


Kama kana kwamba ilikuwa Sukari ya barafu kupamba keki ya sifongo ya Victoria

Sura ya Kumi na Tisa


Kama kana kwamba ilikuwa Sukari ya barafu kupamba keki ya sifongo ya Victoria



















Sura ya Ishirini


Kila wakati mtoto akiniita kwa jina fulani, ndivyo nitakavyoitwa

Sura ya Ishirini


Kila wakati mtoto akiniita kwa jina fulani, ndivyo nitakavyoitwa























Dibaji







"Kila kitu kitakuwa sawa, wewe ni mvulana mkubwa sasa....Rudi na ucheze na Watoto wengine. Tutakutana tena, ninakuahidi''



Mtoto alimtazama akitiririkwa na machozi alipoondoka mtu ambaye amekuwa akicheza naye tangu mwanzoni.



Mtoto alikimbia kurejea kwenye vijigari kwenye bustani iliyojuani, ambako alikwenda kucheza na watoto wengine jirani, huku fikra za rafiki ya kimawazo zikififia polepole.



Baada ya kujipenyeza kwenye mahali watoto wengine walikuwa, hatimaye angeweza kupanda kwa kitelezo. Hakupoteza hata muda na alianza kuteleza kwenda chini ya kitelezo, akisukuma kwa bidii kadri awezavyo. Hakuteleza hata hadi mwisho, wakati alipoona msichana mwenye nywele nyeupe akikimbia kutoka kwa mama yake na kuelekea kwenye miguu yake. Hakuweza kupunguza mwendo na alimgonga kwa nguvu.

 



Msichana huyo mdogo alipoteza mwelekeo na kugonga kichwa chake kwenye ukingo wa kitelezo.



Alijaribu kumfikia mtoto huyo msichana ili kuhakikisha kuwa alikuwa sawa, lakini akasukumwa kando bila huruma na mamaye, ambaye alikuja kumwokoa. Ghafula, kundi la babu na akina mama walikusanyika karibu na msichana huyo maskini.



Alipokuwa akijaribu kutambaa mbali na miguu ya watu wazima, alihisi kwamba alikuwa amezimia. “Mtu mmoja aliita ambulensi!” Huku sauti hiyo ikijitokeza kwa nguvu kwenye maskio yake, alianza kuingiwa na hofu. Alikimbia kuelekea msituni nyuma ya bustani.



Ghafula, kila kitu karibu naye kikawa giza. Upepo baridi ulikuwa umesheheni sauti za kutisha. Mistari asiyoijua ilianza kuchanganyika na mazungumzo ya wazazi kwenye bustani. Zilikuwa zikitoka nyuma ya kundi la miti, ambayo vivuli vyao virefu vilikuwa vinajidhihirisha. Kisha, sauti hiyo ambayo ilikuwa ikijitokeza kutoka pande tofauti ilizidi kuendelea kusikika. Alikuwa akimfikia zaidi na zaidi, hadi alipohisi kuwa ilikuwa ikinong'oneza maskioni mwake:





"Damnabilis ies iom, mirdo cavus mirdo, cessa verunt ies iom, mirdo oblivio ement, mors damnabils ies iom, ospes araneus ies iom…"



Aliweka kichwa chake kwenye mikono yake ili kutuliza sauti hiyo, lakini haikusaidia. Alipiga magoti na akafunga macho yake...





"Damnabilis ies iom, mirdo cavus mirdo, cessa verunt ies iom, mirdo oblivio ement, mors damnabils ies iom, ospes araneus ies iom…"






Sura ya kwanza









Anaepuka nikijaribu kumkumbatia……….







"Elio, Elio, njoo hapa! Nisaidie kuanua mboga kabla ya dharuba kuja, tafadhali."



Elio alikuwa amesimama wima akiwa amevalia viatu vyake vipya na alikuwa akimtazama mamaye, ambaye alikuwa akihangaika katika shughuli zake.



"Elio! Usisimame tu hapo! Chukua hii!" Alimtikisa na kuweka begi iliyojaa mboga kwenye mikono yake. Elio hakuwa na nia ya kufanya kitu kingine. Alipanda ngazi zilizoko nje ya jengo, akageuka na kufungua mlango. Alianza kutazama taa nyekundu ya lifti ambayo mwangaza wake haivumiliki. Kisha, akaacha kusubiri na kupanda ngazi kwenda kwenye nyumba yake gorofani. Aliweka mboga kwenye meza ya jikoni na kwenda moja kwa moja hadi chumba chake cha kulala kusikiza muziki kitandani.



Mara tu alipopanda gorofani mamake akaenda kumtafuta. Alisimama mlangoni akipiga kelele: “Unafanya nini? Hatujamaliza bado, njoo unisaidie!".



"Sawa, nko njiani..." akajibu Elio bila kusonga. Kwa kweli alitaka tu kumwepuka. Giulia akatoka, akitarajia kwamba mara hii itakuwa tofauti. Hakuwa na matumaini. Alikuwa akihangaika kumtia moyo mwanawe, ambaye alikuwa akizidi kuwa mwenye kutojali. Kutoka Mlangoni, aliweza kusikia wazi hatua za dadaye huku akimwita kwa sauti ya furaha. "Elio! Elio! Ondoa makalio kitandani na uje usaidie mama. Anakusubiri huko chini." Alimfokea huku akifahamu kwamba itakuwa bure tu. Elio hakusonga hata inchi moja. Badala yake, aliongeza sauti ya muziki na kuendelea kutazama dari, kana kwamba hakuna kinachotendeka. Giulia, ambaye alikuwa amechoka kutokana na mabishano na mwanawe kuliko kutokana na uchovu, mwishowe alilazimika kupandisha mboga akisaidiana na bintiye, Gaia. Huku akipanda ngazi ya jengo hilo lililo na orofa tano, ambako lifti yaonekana kutofanya kazi kila siku (na kwa kejeli, siku sote haifanyi kazi wakati anapotaka kubeba mboga kupanda ngazi kwenda juu), aliendelea kufikiria kuhusu Elio. Jengo hilo lilipakwa rangi nyeupe na ya machungwa, kama majengo mengine ya baraza la Gialingua, mtaa ambao walikuwa wanaishi. Familia ishirini ziliishi katika mtaa huo, na zilikuwa zimegawanywa katika gorofa ishirini zilizoangalia pande tofauti ya jengo lenyewe.



"Hii ni mara ya mwisho unafanya hivi!" akamfokea akiwa jikoni. "Tutatatua hii punde to baba yako atakaporejea nyumbani!"



Elio hakuwa hata anamsikiliza kwa kuwa alikuwa amezama katika muziki huo wa kuchukiza. Hakuna na hakuna anayeweza kutikisa hisia za uchoshi na ubishi aliousheheni. Dunia yake isiyopendeza ilikuwa kama makazi kwake. Huo ndio ulikuwa utu wake na dunia ililazimika kumzoea. Gaia alikuwa tofauti kabisa: alikuwa na umri wa miaka kumi na mitano, ana macho angavu na nywele fupi nyeusi. Saa ishirini na nne hazikotosha kwake kushughulikia maslahi yake yote.



Giulia alikuwa mwanamke mwenye nguvu pia. Lakini, kinyume cha bintiye, alikuwa na nywele nyeupe zilizopindika, alikuwa mnene kiasi lakini mwepesi na aliyejitolea. Alikuwa mama wa kawaida mwenye umri wa miaka 42: kila wakati alikuwa na ratiba ngumu akijaribu kudumisha usawa kati ya kazi na familia.



Ilikuwa chakula cha jioni. Hata hivyo, hakuna kelele zilizosikika kutoka chumba cha kulala cha Elio. Kwa kweli, hajasonga tangu alipokimbia kujitosa kitandani na kuvaa vipokea sauti vinavyobanwa kichwani.



Alisikia sauti ya ufunguo katika kufuli wa mlango wa mbele. Wakati uo huo, huku mlango ukiwa bado haujafungwa vizuri, sauti ya hamaki ya Giulia tayari ilikuwa imemkera mumewe:



"Hatuwezi kuendelea kufanya hivi!"



"Mpenzi, wacha niingie chumbani kwanza..."



Giulia alimbusu mumewe na kurudi kulalamika.



"Ni kumhusu Elio, sivyo?" alisikika kama aliyekata tamaa wakati alipouliza.



"Ndio, ni yeye." akajibu Giulia.



Wakati uo huo, Carlo akatoa mkebe wa chakula ndani ya begi lake ambalo alikuwa akienda kuacha jikoni. Kisha, alikuwa akienda kuweka mkoba wake kwenye kabati la nguo. Ndani ya mkoba huo, kila wakati angeweka jezi ya ziada kwa kwa sababu ya mawimbi ya joto ambayo yalikuwa yakipiga eneo hilo mwezi huo wa Mei.



Alikuwa mwema, mwenye umri wa miaka arobaini na mbili, mrefu na mwembamba. Nywele zake zilikuwa zimegeuka kijivu, lakini wakati mmoja zilikuwa zinafanana na za bintiye. Uso wake uliochongoka ulikuwa wazi: kwenye pua lake lililofanana na mdomo wa ndege alikuwa akivalia miwani duara ya chuma.



"Tuizungumzie kumhusu baadaye?" kwa upole alimmwuliza bibiye, akitarajia kwamba atasononeka.



"Ndio, uko sahihi mpenzi." alijubu, lakini aliendelea kulalamika hadi wakati chakula cha jioni kilipoandaliwa.



Kwa bahati, Gaia hakuacha kuongea kuhusu siku yake, akichukulia machungu yake madogo kwa njia ya kutia moyo.



Giulia alikuwa amemaliza kuandaa mezani wakati aliposema:



"Umwite Elio."



" Haina maana na unaifahamu." alijibu. "Unajua hatasonga hata inchi moja, isipokuwa aitwe na baba..."



Giulia, kisha akamgeukia mumewe:



"Ameshinda katika chumba hicho tangu nilipomrudisha nyumbani kutoka shule. Anazidi kuwa mbaya."



"Si tulisema atakuwa akirudi nyumbani mwenyewe kuanzia sasa na kuendelea?"



"Nilikuwa katika eneo hilo...



Nilikuwa nikinunua mboga..."



"Kila siku unatoa vizingizio ili kumlinda, lakini tena unalalamika kuhusu tabia yake!"



Carlo alikuwa akitikisa kichwa chake kama ishara ya kutokubali. Kisha, akaamka kwenye kochi na kwenda kwenye chumba cha watoto.



Aliingia kwenye chumba hicho cha kulala bila kubisha hodi na kumpata Elio katika mahali papo hapo ambako Giulia alikuwa amemwacha. Alikuwa akitazama dari kwa macho yaliyofunikwa, na alikuwa bado amevalia vipokea sauti vya maskio vyeupe vya Wi-Fi, na hata alikuwa hajavua viatu vyake.



Carlo hakuamini kwamba alikuwa mvulana yule yule ambaye angeandamana naye kila wakati kwa safari ya kuendesha basikeli. Sasa alikuwa na umri wa miaka kumi na sita, alikuwa mrefu kama yeye, na macho yake ya kijani kibichi bado yalikuwa mazuri, lakini yalionekana yaliyokufa. Katika miaka michache iliyopita, amekuwa akiugua unyongovu. Carlo alikuwa hajasikia kicheko chake kwa muda mrefu, hivi kwamba alikuwa amesahau jinsi inavyosikika. Alikuwa akijuta kwamba hangeweza kukaa naye kwa muda mrefu kama awali. Hata hivyo, alikuwa na shaka kwamba, kufikia sasa, umakinifu wake utathaminiwa.



Kwa bahati mbaya, miaka kadhaa kabla ya hayo, Carlo alikuwa amepoteza kazi yake kufuatia shida za kifedha. Kufuatia kuongezeka kwa mapato, kampuni hiyo ilihamishwa ngambo, kama kampuni nyingine nyingi.



Carlo alijitahidi kupata kazi. Hatimaye, akapata kazi katika mji tofauti. Kila siku alilazimika kusafiri muda mrefu na kubadilisha njia ya usafiri mara kadhaa, na kusababisha kuwa mbali na familia yake kwa saa nyingi kila siku. Hurejea nyumbani akiwa amechoka na akili yake kusubaa. Baada ya chakula cha jioni, analala kwenye kochi na bila shaka kuzama kwenye usingizi licha ya jaribio ya kutaka kuwa macho.



Carlo alidokeza kuwa Elio anapaswa kutoa vipokea sauti vya maskioni. Elio alikubaliana naye tu ili kuepuka kukemewa.



"Ni wakati wa chakula cha jioni. Njoo ule." Aliamuru. "Mamake alisema kuwa umekaa hapa tangu saa kumi jioni!"



Elio aliamka kutoka kitandani, na huku akiangalia chini alitembea kupita mbele ya babaye. Na kisha akatembea kuelekea jikoni, bila hata kujaribu kujadiliana na babaye.



Gaia tayari alikuwa ameketi mezani ambayo alikuwa ameandaa na alikuwa akiwatumia ujumbe rafiki zake na kufanya mipango nao.



Elio aliketi mbele ya dadaye. Walakini hakuongea neno hata moja naye wakati wote wa chakula cha jioni.



Chakula cha jioni kilibainika kuwa kisicho cha furaha. Kila mtu alikuwa akiongea kuhusu matukio yao ya kila siku, isipokuwa Elio, ambaye alikula vipande vichache vya nyama na kurejea kwenye chumba chake haraka iwezekanavyo. Mamaye alisikitishwa na ishara hiyo, na babaye pia ambaye alionekana kukunja uso.



Wakati Giulia na Carlo waliachwa chumbani wakati walikuwa wanaondoa sahani mezani, walianza kuzungumzia mada iyo hiyo ya awali: tabia mbaya za mwanao.



"Ni nini tunafanya vibaya? Hata siwezi kuelewa! Gaia ni mtu tendaji, mwenye furaha na mwenye hiba!" alisema Giulia



"Nilimpuuza sana!" Carlo alijilaumu kama kawaida.



"Wewe si baba pekee duniani ambaye analazimika kuwa mbali na nyumbani kwa saa nyingi. Mimi, kwa upande mwingine, niko nyumbani kila alasiri" Alirudia tena kwa kuwa hakutaka mumewe kuhisi kuwa na mzigo begani.



"Sio swala la tabia, Giulia, kwa sababu Elio hakuwa hivi awali, na unaijua!"



"Natamani pia kwamba asingekuwa hivi, Carlo, lakini watoto hubadilika wanapokua. Na kisha, wanazidi na kuzidi kuwa wabaya zaidi, sivyo? Akiwa shuleni ni balaa. Natarajia kuwa hatapinga, lasivyo hatutaweza kumpeleka kwenda kambi ya majira yajayo ya joto...hatutaweza kumruhusu kwenda shule wakati wa kiangazi...hatafurahia!"



"Giulia, watoto wengine kwa kawaida huburudika shuleni wakati wa kiangazi. Watoto wa Francesca na Giuseppe wanafurahia sana. Unafahamu vyema kuwa hatafanya chochote kwenye kambi ya majira ya joto! Tunahitaji kutafuta chaguo jingine, kitu ambacho kitamfanya apambane. Hata haonekani kuwa na furaha. Je! Unakumbuka jinsi tulivyokuwa na nguvu wakati tulipokuwa na umri sawa na yake?"



"Bila shaka, naikumbuka!" Mamangu angefoka kwenye mlango wetu kwamba chakula cha jioni kimekuwa tayari. Lakini, mara nyingi, hata singemsikia kwa kuwa nilikuwa na shughuli nyingi kwenye bustani nikijibingirisha kwenye nyasi. Tulikuwa na furaha na huru. Kwa kweli hatuwezi kumpa maisha kama hii mjini. Walakani, hajui jinsi ya kufurahia kambi ya majira ya kiangazi. Hana rafiki, hakuna tunayeweza kumwalika na kumsaidi kuponya tabia hii ambayo anaishi. Haruhusu mtu yeyote kushikamana naye. Wakati mwingine najiuliza jinsi anavyohisi kuhusu sisi. Anakwepa ninapojaribu kumkumbatia..."



"Giulia, vijana hawataki kukumbatiwa na mama zao. Nina uhakika bado anatupenda, lakini hatuwasiliani naye kwa njia mwafaka. Tunahitaji kutafuta njia mpya. Tunahitaji kutafuta njia ya kumuamsha. Labda, angezungumza na Ida? Ana wavulana wawili wadogo. Labda anaweza akatupatia ushauri mzuri. "



"Unaogopa anaweza geuka kuwa kama Libero? Kwamba anaugua ugonjwa unaorithiwa wa kisaikolojia?"



"Hapana, kwa Libero ilikuwa tofauti. Matatizo yake yalitokana na kifo cha babaye. Lakini matukio hayo yanafanana na jinsi Ida anavyofahamu huenda ukafaa. Alifanya miujiza na kijana huyo baada ya kuhamia kijijini. Na alifanya yote hayo pekee yake! na shamba ilisaidia pia."



"Ndio, umjulishe hayo. Naamini dadako. Ana njia yake ya kuangalia mambo, na ninapenda."



"Tutaipata ripoti ya shule lini?" Carlo akamwuliza bibiye.



"Juni 19..."



"Tutakuwa tumechelewa kuamua kitu cha kufanya. Unapaswa kuuliza mwalimu wake wa Italia kuwa na mazungumzo ya moja kwa moja na wewe. Lazima tuamue ni wapi tunapeleka watoto wetu. Maombi ya kujiunga na kambi ya majira ya kiangazi na shule ya majira ya kiangazi yatafungwa kabla ya tarehe 19." alipendekeza Carlo.

 



"Ndio, umesema ukweli. Tunahitaji kuwa na uhakika wa hali hiyo, ingawa hafanyi vibaya shuleni. Ni vile tu haweki royo yake katika chochote anachokifanya. Unafahamu kwamba wapangaji wapya wameingia orofa ya pili? Waonekana kuwa watu wazuri. Bi Giovanna aliniambia walihamia hapa kutoka Potenza. Hiyo ni mbali! Hakika haitakuwa raisi kwao mwanzoni. Wana mwana aliye na umri sawa na Elio. Nitamwalika aje mchana fulani..."



Giulia kisha akagundua kuwa Carlo, ambaye alikuwa amelala kwenye kochi, tayari alikuwa amezama usingizini.



"Njoo, mpenzi, twende tukalale kitandani." Alimnongoneza kwa upole ili amwamshe.






Sura ya pili









Mnong'ono wa baridi ulikuwa ukimsumbua







Elio alikuwa amesimama kwenye njia pana ya miguu mbele ya shule yake. Watoto wengine wote waliokuwa karibu naye walikuwa wakiongeza kasi, wanaposhuka katika gari za wazazi wao au wakifukuzana wakiwa njiani kwenda nyumbani. Yeye kwa upande mwingine alikuwa akiangalia kila mahali kwa wasiwasi kwa gari ya mama yake kana kwamba ndio njia yake ya kuishi, akitarajia kwamba hajaondoka baada ya kukutana binafsi na mwalimu wake wa Italia.



Baada ya kila mtu kuondoka katika yadi ya shule kwa muda mfupi, Elio aliacha kusubiri na kuanza kutembea kwenda nyumbani. Alichukia kutembea. Na alichukia hata zaidi kutembea chini barabara hiyo isiyovumilika iliyo na mstari wa miti ya ndimu inayounganisha shule na nyumba yao.



Alisubiri dakika chache zaidi na kisha akaamua kuelekea nyumbani pekee yake. Kisha, akamuru mguu wake kusonga mbele. Kwa mtu mwengine yule inaweza kuonekana kama kazi raisi, lakini kwa Elio, ambaye mawasiliano yake na miguu yake ilikuwa haba, ilikuwa mapambano.



Akageuka kushoto kupitia del Corso; akiwa kwa kona alijipata mbele ya barabara iliyonyooka ambayo aliidharau. Kijisitu cha miti ya ndimu ilipandwa kando kando ya barabara hiyo kuu. Kwa mtu mwengine yule ilikuwa tu kijisitu kizuri cha miti ya ndimu iliyochanua ambayo manukato yake yalibebwa na upepo, na kulifanya eneo hilo kunukia viruzi. Alipoanza kwenda chini kufuata mistari ya miti kwa ugumu, alihisi kuwa anafuatwa.



Aligeuka kwa haraka na kufikiria kuwa alikuwa ameona mnyama mweusi amejificha nyuma ya mti.



"Haiwezi kuwa" aliendelea kujirudia mwenyewe. "Je! Nimeona miwani katika pua la mbwa huyo wa ajabu?"



Kwa hofu akaendelea kutembea, huku akiona vivuli nyuma ya miti. Isitoshe, upepo ulikuwa ukivuma kupitia matawi. Mnongono wa upepo ulikuwa unamhangaisha; ilikuwa ikikuna maskio yake na kisha kukwama kwenye akili yake.



Hakuweza kuelewa maana ya sauti hizo. Huku akiwa ameshikwa na hisia hiyo mbaya, aliamuru mwili wake kujaribu na kukimbia. Alikuwa akitokwa na jasho, na akikimbia zaidi, sauti hizo zilizidi kuonekana kama zinamkimbiza na vivuli vikaonekana kuzidi kumkaribia.



Alianza kukimbia kwa kasi na kwa uwezo wake wote. Kisha, alisikia sauti ya kikatili ikimwamuru kuacha kukimbia. Aligeuka mara moja na kwa mara nyingine aliona kitu ya sura nyeusi ikijificha nyuma ya mti uliokaribu. Alikuwa tayari amefika makutano na barabara kuu, ambayo ingeashiria mwisho wa ndoto hiyo.



Hata hivyo, alihisi upepo baridi nyuma ya shingo yake. Aligeuka tena, mara hii bila kukimbia, lakini kitu kilimgonga vikali na kumtupa chini.



Elio alishtuka na kujikunja kama mpira huku kichwa chake kikiwa kwenye mikononi mwake.



Wakati uo huo, alisikia sauti anayoijua ikimwita:



"Elio! Elio! Je! Unafanya nini?"



Ilikuwa dada yake ambaye alikuwa akimkaripia. Alikuwa amekasirika kwa kuwa alikuwa amemkimbilia. Baadaye alitambua kuwa Elio alikuwa katika hali mbaya.



Alitulia na kuuliza:



"Unajisikiaje?"



Elio, baada ya kusikia sauti yake, akainua kichwa chake.



Gaia aligunduwa kuwa alikuwa amechanganyikiwa, anatoa jasho na uso wake ulikwajuka kuliko kawaida. Kwa sekunde, alijaribu kufikiria ni kwanini alikuwa akikimbia. Haikuwa kawaida kwake. Ilionekana kwake kwamba alikuwa akitoroka kitu au mtu. Wakati uo huo, alimsaidia kuinuka.



"Kwanini ulikuwa ukikimbia hivyo?" alimwuliza. "Kuna kitu kilikutisha?"



Gaia hakukumbuka mara ya mwisho Elio alikimbia. Elio hakujibu. Kitu pekee alichokitaka ni kuondoka barabarani haraka iwezekanavyo. Alipiga kona barabarani bila kusema lolote.



Gaia akamfuata akiwa na wasi wasi.



"Elio!" alimwita tena.



"Hakuna kitu!" akajibu Elio kwa ujeuri. "Kwa kweli hakuna kitu!"



Tabia ya Elio ilimfanya Gaia kukasirika tena.



"Hakuna kitu, eeh? Ulinikimbia sawasawa. Na bado, unasema hakuna kitu!"



Elio alimwomba msamahaili kuepuka majadiliano zaidi, only to avoid further discussions, ambayo ingechosha mwili wake hata zaidi.



"Samahani." alisema.



Misamaha hiyo ya juu juu iliishia kumkasirisha Gaia hata zaidi. Hata hivyo, aliendelea kutembea nyuma ya kakaye, huku akiwa na wasiwasi kumhusu.





Kufikia Jumapili asubuhi, Carlo na Giulia hatimaye walikuwa wamefanya uamuzi. Wakati walipokuwa wanatengeneza kiamsha kinywa, walikuwa wakiongea kuhusu wazo hilo wakati wakisubiri watoto kuamka



"Alikuwa mkarimu kutoa wazo kama hilo. Nataraji, hao watato watakuwa na tabia njema." alisema Giulia akiwa na tabasamu kubwa usoni.



Ilikuwa uamuzi ngumu kufanya, lakini Carlo na yeye walikuwa wanahisi shauku ya ajabu kuihusu, kwa vile walikuwa wamekubaliana nayo.



"Gaia atafurahi." alisema Carlo. "Elio, kwa upande mwingine, atasalia kutojali kama kawaida."



"Sina uhakika...Gaia alifanya urafiki na watoto wengine katika kambi ya majira ya joto. Atakasirika. Na kuhusu Elio, atachukia hata hivyo." akasema Giulia.



"Siwezi kusubiri tena. Nitawaamsha." akapendekeza Carlo kwa uthabiti, na kutembea kwenda vyumba vyao akiwaita kwa majina yao.



Hakuniruhusu hata kusafisha uso wao.



"Mama yako na mimi tuliamua kile utakachofanya wakati wa majira ya joto. Shule itafungwa Ijumaa na Jumapili Asubuhi mtapelekwa kwa kituo cha reli!"



"Lakini kambi ya majira ya joto haitaanza kwa majuma mengine mawili yajayo!" Gaia alisema kwa wasi wasi na kumtazama mama yake. Kutoka mlango wa jikoni, alikuwa akitazama kile kilichokuwa kikiendelea kwenye ushoroba.



"Kwa kweli, hutaenda kwenye kambi ya majira ya joto mwaka huu" akajibu Giulia na kwa kufanya hivyo, alithibitisha hofu ya Gaia. "Tulifikiri tutakupa fursa ya kutumia wakati wako wa majira ya joto kwa mtindo wa zamani; jinsi tulivyofanya wakati tulipokuwa na umri kama yako. "



"Hiyo inatakikana kumaanisha nini?" akauliza Gaia, wakati Elio alikuwa kimya na mwenye sura mbaya.



"Utakuwa nje, kimbia hadi upungukiwe na pumzi, ogelea kwenye bwawa na utumie usiku wa majira ya joto kwenye maonesho mtaani" akajibu Carlo kwa bintiye.



Gaia aliweza kuona wazazi wake wakiangaliana na kucheka, na kwa haraka akafikiria walikuwa wakiwafanyia mzaha.



"Acha kutufanyia mzaha. Mnashida gani asubuhi hii?"



"Hiyo si mzaha. Shangazi Ida amejitolea kuwakaribisha wakati wa majira ya joto." Hatimaye Carlo akafichua kwa watoto wake, ambao walikuwa wakimwangalia bila kuamini.



"Hii ni ndoto mbaya. Ninarudi kulala!" akasema Gaia, ambaye alionekana kukasirika.



"Nilifikiria utafurahi " akasema babaye.



"Kufurahi? Tayari nilikuwa nimewasiliana na rafiki zangu! Nimesubiri wakati wote wa msimu wa baridi!"



"Gaia, utapata rafiki kwa shangazi pia." Mtie moyo Giulia.



"Lakini kwanini nitake kufanya hivo? Ninapenda kuwa na rafiki katika kambi ya majira ya joto. Ninaweza kukaa nje na kupiga mbizi ziwani. Sitaki kuwa mahali pengine."



"Ndio, hutaki. lakini Elio anataka. Anahitaji kubadilisha hewar." Akaongeza Carlo.



"Nilijua!" akaropoka. "Ni kwa sababu ya Elio! Na mbona asiende kwa shangazi Ida pekee yake?"



"Hatutaki aende pekee yake." akasisitiza Giulia.



"Mimi si yaya wake!"



"Lakini wewe ni dada yake mkubwa. Mbona husemi kitu, Elio?" akauliza Carlo.



Elio hakusema lolote. Akainua mabega yake, na kuathiri akili ya Gaia.



"Hivyo? Hakuna? Hakuna swala muhimu wkako. Haya! ambia mama na baba kwamba hutafanya chochote shambani pia."



Elio aliinama na kukubaliana naye.



"Acha, Gaia! Acha kufanya hivi! Tayari tumeshaamua. Binamu yako Libero atakuchukua kituoni" tamatisha mazungumzo Carlo.



Gaia akakimbia, akionekana kufa moyo na kukasirika.



"Atakuwa sawa." akasema Giulia, akijua starehe ya maisha ya bintiye.



Elio alirudi kwenye chumba chake bila kutambuliwa.



Carlo alishangaa. Hata hivyo, alikuwa na uhakika kwamba uamuzi wao ulikuwa bora katika kwa miaka mingi.





Ijumaa ilifika haraka. Carlo alimchukua mpwa wake kutoka kituoni na kufurahi alipofikiria kumkumbatia tena.</p